10 Mei 2025 - 23:30
Ayatollah Sheikh Jawadi Amuli Atembelea Makao ya Maimamu wa Ahlul-Bayt (as) Samarra, Akaribishwa kwa Heshima Kubwa

Katika heshima ya ziara hii tukufu, Haram ilifanya hafla maalum ya kumuenzi Sheikh Jawadi Al-A'muli, sambamba na kuzinduliwa kwa kitabu chake kipya chenye kichwa: Sharh Ziyarat Al-Jami'a Al-Kabira

Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) -ABNA-Uongozi Mkuu wa Haram Tukufu ya Askariyayn umempokea kwa heshima kubwa Kiongozi wa Dini, Marjaa wa Kiislamu Ayatollah Sheikh Abdullah Jawadi Al-A'muli, baada ya kupata fursa ya kutembelea Makaburi Matukufu ya Maimamu wawili wa Ahlulbayt (as), Imam Al-Askari na Imam Al-Hadi (amani iwe juu yao) pamoja na sehemu tukufu ya Sardab, iliyopo katika mji wa Samarra.

Ayatollah Sheikh Jawadi Amuli Atembelea Makao ya Maimamu wa Ahlul-Bayt (as) Samarra, Akaribishwa kwa Heshima Kubwa

Katika heshima ya ziara hii tukufu, Haram ilifanya hafla maalum ya kumuenzi Sheikh Jawadi Al-A'muli, sambamba na kuzinduliwa kwa kitabu chake kipya chenye kichwa: 

Sharh Ziyarat Al-Jami'a Al-Kabira (Ufafanuzi wa Ziara ya Jami'a Kubwa), riwaya ya Imam Al-Hadi (amani iwe juu yake).

Ayatollah Sheikh Jawadi Amuli Atembelea Makao ya Maimamu wa Ahlul-Bayt (as) Samarra, Akaribishwa kwa Heshima Kubwa

Wakati wa hafla hiyo, zawadi zenye baraka zilitolewa kwa Ayatollah Sheikh Jawadi A'muli, ikiwemo bendera ya Maqam wa Ma-Imamu Wawili Askariyayn, kama ishara ya kutambua juhudi zake kubwa katika elimu ya Dini. 

Ayatollah Sheikh Jawadi Amuli Atembelea Makao ya Maimamu wa Ahlul-Bayt (as) Samarra, Akaribishwa kwa Heshima Kubwa

Kwa upande wake, Sheikh Al-Amuli aliikabidhi Haram nakala ya kitabu chake kipya kwa ajili ya matumizi ya watafiti katika Mji Mtukufu wa Samarra.

Tags

Your Comment

You are replying to: .
captcha